Saturday, November 3, 2012

"NATAKA KULEWA" NI WIMBO WANGU NA HATA DIAMOND ANAJUA. LAKINI AMEAMUA KUNIIBIA



(H- baba akiwa ameshika cd ya demo yenye wimbo huo kama ushahidi)

Namshangaa sana huyu bwana mdogo, alikuja studio kwa Maneke akiwa na Sheta wakati wanafanya ngoma yao ya nidanganye, wakanikuta mimi na Q chillah tunafanya wimbo wangu mpya (nataka kulewa) ambao nimemshirikisha Q chillah kwenye kiitikio. Diamond akasema ameupenda huo wimbo na akawa ananiambia nimuimbie kwani unamfurahisha nami nikawa namuimbia. Leo nasikia kautoa redioni wakati mimi sijamaliza kuuredi. Kama mnabisha muulizeni Q chillah au maneke. "hayo ndiyo malalamiko ya msanii Hamisi baba ambaye ni mkongwe kwenye fani ya muziki wa kizazi kipya. Pia aliendelea kusisitiza kuwa kitendo cha Diamond kuiba baadhi ya maneno katika kiitikio na jina la wimbo huo kimemsikitisha sana



No comments:

Post a Comment