Monday, November 5, 2012

TUHUMA ZA DIAMOND PLATNUMZ KUIBA WIMBO WA H-BABA. Q CHIEF AFUNGUKA KUTOA USHUHUDA




Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, raia wa Tanzania al maarufu kama mzee wa kubembeleza Q chillah. Aliyetajwa kama shahidi katika malalamiko ya H-baba kuibiwa songi lake la "Nataka kulewa" na msanii Nassib Abdul (DIAMOND). Juzi kati mtu mzima Chillah alivunja ukimya alipokuwa akihojiwa na Radio ya watu Clouds fm na kutiririka. "Ni kweli tulikuwa katika maandalizi ya kurekodi wimbo huo na H-baba na mimi ndiye niliyeimba kiitikio na hata Diamond na Sheta walipokuja wakakuta tunaimba na kuupenda wimbo, lakini kwanini tugombane au kuanzisha mzozo kwa sababu ya wimbo? labda mawazo yaligongana tu. H-baba ni msanii mkubwa naamini ana uwezo wa kufanya ngoma nyingine." Alisema Q Chief.

kama umeusikia wimbo nataka kulewa wa Diamond ambao umezua utata basi ni nafasi yako kuusikia na wa H-baba ambaye analalamika kuibiwa wimbo huo ambao bado haujakamilika, kisha utapima mwenyewe.

 Banyoza HAPA kusikiliza


No comments:

Post a Comment