Friday, December 28, 2012

HAPPY BIRTHDAY TO GOSSIP COP, MHARIRI MKUU WA GAZETI LA MAKOROKOCHO "SUDI BROWN"







Kwa wale wasikilizaji wa the people station Clouds fm na ambao ni mashabki wa kipindi cha XXL bila shaka huwa wanasikia au kusikiliza jinsi team makorokocho kupitia gazeti lake la Makorokocho likiwa linawasilisha tetesi za mtaani kila siku mida ya mchana kwenye kipindi hicho.

 Kwa niaba ya The Dj Max Entertainments na wapenda burudani wote bila ya kusahau mashabiki wa clouds fm tunampongeza Producer Soud Brown kwa kutimiza miaka kadhaa siku ya leo. Tunamuombea maisha marefu na yenye baraka. Pia tunamuombea Mungu amjaalie kizazi apate watoto wengi sana ili kufanikisha kujaza dunia "Samahani lakini" si kwa ubaya!!!!!

          YOU HEARD???????

Thursday, December 20, 2012

BREAKING NEWS!!!! Q CHIEF ATANGAZA RASMI KUACHANA NA MADAWA YA KULEVYA NA KUWAOMBA RADHI MASHABIKI WAKE NA KUTOA NGOMA MPYA





Kama wewe ni shabiki wa muziki wa kizazi kipya ndani ya Afrika Mashariki bila shaka jina Q-chillah wala haliwezi kuwa geni masikioni mwako. Mwanamuziki huyu kutoka jiji Da es Salaam Tanzania, leo amekiri ndani ya kipindi cha xxl cha Clouds Radio alipokuwa akipiga stori na Adam Mchomvu "BABA JONII"  kuwa alikuwa akitumia dawa za kulevya kwa takriban miaka miwili na kwa sasa ameacha kutumia kwa zaidi ya miezi saba.

Ingawa hakuweka wazi ni dawa zipi alikuwa akizitumia na kwa njia zipi lakini alisema kwa sauti ya kusikitisha kuwa "kaka we acha tu nimepitia mengi". Pia alikuwa akikataa kujibu baadhi ya maswali kwa kile alichokieleza kuwa akiongelea swala hilo linamletea kumbukumbu mbaya ambazo hapendi kuzikumbuka kwa sasa.

Pia alichukua nafasi hiyo kuwaomba msamaha mashabiki wake, ndugu jamaa na marafiki endapo alikuwa amewakosea kwa tabia hiyo aliyokuwa nayo kipindi hicho. Alisisitiza kuwa amefanya maamuzi ya kuacha uteja kwa ajili ya watoto wake na wazazi wake pia, kwani anaamini kuwa aliwaumiza sana.

HONGERA SANA CHILLAH

VIDEO NYINGINE MPYA KUTOKA KWA DIAMOND PLATNUMZ INAITWA KESHO

Sunday, December 16, 2012

NEW VIDEO "ANOTHER CHANCE" BY BOBBY ST ft DERRICK WALUUBE

BREAKING NEWS!!!!! FC SCHALKE 04 WAFUKUZA MAKOCHA




Baada ya kutofanya vizuri kwenye ligi kuu ya soka nchini Ujerumani Bundesliga, uongozi wa timu ya Fc Schalke 04 umekatisha mkataba rasmi leo kwa njia ya amani na makubaliano na aliyekuwa kocha wa timu hiyo bwana Huub Steven. Uamuzi huo ni kufuatia timu hiyo kutopata ushindi katika michezo 7 mfulizo ya Bundesliga. Pia wamemtimua kocha msadizi na kwa sasa nafasi ya ukocha inashikiliwa na aliyekuwa kocha wa timu ya watoto chini ya umri wa miaka 17 wa timu hiyo.



THE NEW AFRICAN SONG MEKXO FT MARLAW "NWA BABY"

GERMAN SUPER TALENT AND THE WINNER IS.......!


                                        JEAN-MICHEL AWEH

German Super Talent 2012



A congoleese man Christian Bakotessa from Ngoma Africa Band (Bremen Germany) on the second place in German Super Talent 2012

                                                 
 

Friday, November 30, 2012

KITALE AWALAANI WALIOMFANYIA UBAYA SHARO MILIONEA



Swahiba wa karibu wa marehemu "Sharo" na pia ni mshirika wake mkubwa kwenye kazi za muziki na sanaa ya uchekeshaji "Kitale" Juzi alilaani vikali na kuwalaani waliomfanyia vitendo visivyo vya kibinaadam Sharo baada ya kupata ajali. Kitale aliongea kwa masikitiko na uchungu mkubwa alipokuwa akihojiwa na Millard Ayo wa Clouds Fm, "Watanzania hawana huruma, wamemvua marehemu mpaka viatu yani wamemuacha na nguo ya ndani tu" hayo ni baadhi ya maneno aliyoyasema Kitale.

Kiukweli kabisa kitendo hicho hakina hata chembe ya uungwana hasa ukizingatia ajali mbaya kama hiyo aliyoipata Sharo, watu badala ya kufika eneo la tukio nakutoa msaada badala yake wanaenda kufanya vitendo vya wizi na uhalifu. Pia kitale alisema kuwa marehemu wakati anaondoka alikuwa na jumla ya shilingi za kitanzania milioni 6 ambazo pia hazikupatikana. Huku akiwa na sura iliyojaa machungu kitale aliongea maneno hayo kwa huzuni alihani kana kwamba haamini kama ni kweli kampoteza swahiba wake.

Kwa niaba ya " THE DJ MAX ENTERTAINMENTS" tunaungana na kitale na waungwana wengine wote kulaani kitendo kisicho cha kibinadamu alichofanyiwa marehemu "Sharo".Pia tunalaani matendo kama hayo katika ajali nyinginezo. Vilevile tunatoa pole kwa Familia ya wafiwa, ndugu jamaa na Marafiki. Mungu ailaze pema roho ya Marehemu. Ameen!

Saturday, November 10, 2012

EPIQ BONGO STAR SEARCH!!! AND THE WINNER IS WALTER CHILAMBO



Ni mzaliwa wa Mbeya na aliyekulia na kusomea mkoni humo, lakini alikuwa akiwakilisha mkoa wa Dar es Salaam katika shindano la kuimba la "Bongo Star Search" ambalo limefikia kilele masaa machache yaliyopita. Hakuna ubishi wala utata kuwa huyu ndiye mshindi na amejinyakulia kitita cha shilingi za kitanzania milioni 50  ikiwa inakaribia sawa na dola za kimarekani 50,000/=

HONGERA SANA WALTER 



Monday, November 5, 2012

MATONYA'S NEW VIDEO "ZILIPENDWA"

TUHUMA ZA DIAMOND PLATNUMZ KUIBA WIMBO WA H-BABA. Q CHIEF AFUNGUKA KUTOA USHUHUDA




Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, raia wa Tanzania al maarufu kama mzee wa kubembeleza Q chillah. Aliyetajwa kama shahidi katika malalamiko ya H-baba kuibiwa songi lake la "Nataka kulewa" na msanii Nassib Abdul (DIAMOND). Juzi kati mtu mzima Chillah alivunja ukimya alipokuwa akihojiwa na Radio ya watu Clouds fm na kutiririka. "Ni kweli tulikuwa katika maandalizi ya kurekodi wimbo huo na H-baba na mimi ndiye niliyeimba kiitikio na hata Diamond na Sheta walipokuja wakakuta tunaimba na kuupenda wimbo, lakini kwanini tugombane au kuanzisha mzozo kwa sababu ya wimbo? labda mawazo yaligongana tu. H-baba ni msanii mkubwa naamini ana uwezo wa kufanya ngoma nyingine." Alisema Q Chief.

kama umeusikia wimbo nataka kulewa wa Diamond ambao umezua utata basi ni nafasi yako kuusikia na wa H-baba ambaye analalamika kuibiwa wimbo huo ambao bado haujakamilika, kisha utapima mwenyewe.

 Banyoza HAPA kusikiliza


Saturday, November 3, 2012

"NATAKA KULEWA" NI WIMBO WANGU NA HATA DIAMOND ANAJUA. LAKINI AMEAMUA KUNIIBIA



(H- baba akiwa ameshika cd ya demo yenye wimbo huo kama ushahidi)

Namshangaa sana huyu bwana mdogo, alikuja studio kwa Maneke akiwa na Sheta wakati wanafanya ngoma yao ya nidanganye, wakanikuta mimi na Q chillah tunafanya wimbo wangu mpya (nataka kulewa) ambao nimemshirikisha Q chillah kwenye kiitikio. Diamond akasema ameupenda huo wimbo na akawa ananiambia nimuimbie kwani unamfurahisha nami nikawa namuimbia. Leo nasikia kautoa redioni wakati mimi sijamaliza kuuredi. Kama mnabisha muulizeni Q chillah au maneke. "hayo ndiyo malalamiko ya msanii Hamisi baba ambaye ni mkongwe kwenye fani ya muziki wa kizazi kipya. Pia aliendelea kusisitiza kuwa kitendo cha Diamond kuiba baadhi ya maneno katika kiitikio na jina la wimbo huo kimemsikitisha sana



Thursday, November 1, 2012

ALICHOKIONGEA BOB JUNIOR KUHUSU NGOMA MPYA YA DIAMOND "NATAKA KULEWA"




"Ni wimbo wa kawaida sana wala sijaona mabadiliko wala ubunifu, bila kuambiwa hata wewe utajua tu kuwa ni nani anaeimba". Maneno hayo aliongea rais wa Masharobalo na Bosi wa Sharobalo records bwana Bob Junior, alipokuwa akifanya mahojiano na Soud brown wa Clouds Fm. kwenye kipindi cha xxxL. Pia aliongeza kwa kusema kwa sasa nipo tayari kupimana nae nae uwezo kwani watu sio wajinga waangalia kipaji na sio majigambo

DAVID ALABA KUFUNGUA KESI DHIDI YA KITUO CHA T.V CHA "ORF" KWA KUMDHALILISHA



Mchezaji kinda ndani ya nyota nyekundu ya kusini "FC BAYERN" raia wa Austria mwenye asili ya mchangiko wa kiafrika na Asia (baba kutoka Nigeria na mama kutoka Ufilipino). David Alaba amepeleka malalamiko kwa mwanasheria wake na kutaka kufungua kesi dhidi ya kituo hicho cha nchini Austria kwa kitendo ambacho alikiona ni cha kudhalilisha na kumbagua. Kupitia kipindi chake cha Commedy, walimuonyesha mtu mweusi mwenye jezi ya Bayern akiwa na tajiri wa kizungu kutoka Canada.

Matukio yaliyomkera Alaba ni pamoja la tajiri huyo kumuonyesha ndizi (chakula cha nyani) Alaba, pia kumuuliza kama anaishi kwenye nyumba za ukimbizi au nyumba za mabati zilizoezekwa na nyasi. Pia mtu huyo alimuuliza Alaba kama ana elimu au amewahi kwenda shule kwa kuwa "Black man" anawaza hela tu. Hata hivyo kituo hicho cha TV kiliomba radhi kwa mchezaji huyo na kuweka wazi kuwa hawakuwa na lengo la kumdhalilisha. Mpaka sasa Alaba hajaonyesha bado dhamira yoyote ya kubadili msimamo wake juu wa kufungua kesi dhidi ya televisheni hiyo



Monday, October 29, 2012

WIMBO MPYA WA DIAMOND "nataka kulewa" BONYEZA HAPA KUSIKILIZA

HONGERA J4 KWA KUCHUKUA JIKO



J4 akiwa na mwandani wake baada ya kufunga pingu za maisha katika pozi lenye tabasamu la nguvu kwa furaha


Chanda chema huvishwa pete, kwa uzima na ugonjwa mpaka kifo



Wadau wa Augsburg nao waliwakilisha, kutoka kulia Malumbo S Malumbo (mambo bado Sounds), Othman Babu (Black Mamba) bwana harusi na bibi harusi.


Monday, October 22, 2012

CHEGE CHIGUNDA AKANUSHA KUMTIA MIMBA MKE WA MTU



Msanii mwenye jina kubwa ndani ya bongo kutoka mitaa ya Temeke jijini Dar es Salaam leo alifunguka alipokuwa akipiga "story" na kipindi cha XXL cha clouds fm. Chege alikanusha vikali tuhuma au uzushi huo uliokuwa umezagaa kila kona baada ya kubainika kuwa mtu huyo hakuwa na ushahidi sababu ambayo imempelekea Chege kusema kuwa atachukua hatua na taratibu za kisheria dhidi ya mtu huyo


Friday, October 19, 2012

OGOPA DEEJAYZ NDIO WATAKAO HUSIKA KATIKA KUANDAA VIDEO YA WIMBO MPYA WA TUNDA MAN



Msanii kutoka kundi la Tip Top Connection lenye maskani yake maeneo ya Magomeni jiji Dar es Salaam "Tunda Man" leo aliamua kufunguka kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa "Face Book". Tunda aliamua kuwatoa hofu mashabiki wa masongi yake yake kwa kuandika kuwa ngoma mpya tayari imekamilika kwa upande wa sauti na kinachofuata ni video ambayo itafanywa nchini kenya na wakali wa siku wa muziki wa Afrika Mashariki "Ogopa Deejayz". Alimalizia kwa kusema kaeni mkao wa kula, mambo matam na mazuri yanakuja.

Thursday, October 11, 2012

KITENDO CHA DIAMOND KUVUA NGUO ON THE STAGE,... NINI TAFSIRI YAKO???



Gumzo lililopo kwa wadau wengi wa burudani ni kwa sasa ni juu ya kitendo cha msanii wa Bongo Fleva ambaye anashika chati ya juu kwa sasa "Diamond Platnumz" Nassib Abdul kushusha suruali yake mpaka chini na kubaki na nguo ya ndani kisha kuwapa mashabiki mgongo na kuinama.

Habari hii yazungumziwa sana kutokana na baadhi ya wasanii wa Bongo movi kukutwa na matukio kama hayo katika kipindi cha hivi karibuni na kukemewa vikali sana na baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya (bongo fleva). Jumamosi iliyopita katika kilele cha Tamasha la Fiesta jijini Dar es Salaam baadhi ya mashabiki hawakuamini macho yao baada ya msanii Diamond kufanya kituko hicho.

Kila mtu kwa upande wake anazungumzia tofauti kituko hicho, kuna gazeti lilidiriki kuandika eti kuwa amemuiga mpenzi wake wa zamani "Wema sepetu" kwani naye pia aliwahi kupatwa na mkasa kama huo kwa kuonesha baadhi ya sehemu za makalio yake kwenye jukwaa la Fiesta mwka jana. Pia kuna waliosema kuwa labda anamuiga afande sele kwani pia aliwahi kufanya kituko kama hicho miaka kadhaa iliyopita katika ukumbi wa Diamond Jubilee. Na kuna mdau aliyeandika kwenye ukurasa wake wa face book " ah Diamond kama 50 cent"

JE WEWE MDAU TAFSIRI YAKO NINI???


HUYU JAMAA ANAUCHUNGU NA YANGA KULIKO HATA WEWE

Tuesday, October 9, 2012

Friday, October 5, 2012

MASIKINI LULU!!!! ARUDISHWA TENA LUPANGO NA KESI YAKE YAANZA UPYA




Elizabeth Michael (LULU)

Akiwa chini ya ulizi wa jeshi la polisi na kuhifadhiwa rumande kwa miezi kadhaa kutokana na tuhuma zinazomkabili za kusababisha kifo cha msanii mwenzie Steven Charles Kanuma. Msanii "lulu" leo alijikuta katika wakati mgumu baada ya mahakama ya rufaa kuamua kuwa kesi yake irudishwe mahakama ya kisutu na kuanza kusikilizwa upya kutokana na kutofuatwa kwa baadhi ya taratibu, ambapo Naibu msajili wa mahakama ya rufaa Bi Zahra Marume alitoa ufafanuzi huo masaa machache yaliyopita wakati kesi hiyo ilitarajiwa kusikilizwa na kushindikana. 

HUYU JAMAA MZIMA KWELI HUYU????

Sunday, September 30, 2012

BAADA YA KIMYA KIREFU "CHIDI BENZ" AFUNGUKA

MUANZILISHI WA BONGO FLEVA APATA MTOTO



Miongoni mwa wasanii wa awali kabisa kutambulika katika ramani ya muziki wa kizazi kipya mwanzoni mwa miaka ya tisini, Joseph Mbilinyi "Mr too proud au Sugu" ambaye kwa sasa ni mbunge wa jimbo la Mbeya mjini kupitia chama cha Chadema. Sasa amekuwa baba baada ya mwenyezimungu kumjaalia neema ya mtoto.

Pia ifahamike kuwa Sugu ndio msanii mwenye Album nyingi zaidi kuliko kuliko msanii mwingine yoyote wa bongo fleva. Vilevile ni msanii wa kwanza kutoa album na ndiye aliyekuwa msanii wa kwanza wa bongo fleva kupata nafasi ya kupiga "show" barani ulaya



Huyu ndiye mtoto wa Sugu, kwa jina anaitwa Sasha. Mungu ambariki na kumkuza vizuri


Thursday, September 27, 2012

RICK ROSS KUFANYA BONGE LA SHOW DAR ES SALAAM




Habari zilizothibitika muda mchache uliopita zinasema kuwa msanii kutoka nchini Marekani "Rick Ross" ndiye msanii wa kigeni atakayetumbuiza kwenye kilele cha Tamasha la Fiesta linaloandaliwa na Clouds Media, linalotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 6 Oktober 2012.

Wednesday, September 26, 2012

FILAMU MPYA YA MAREHEMU KANUMBA SASA IPO MADUKANI




Ikiwa ni miezi kadhaa imepita tangu kifo chake, aliyekuwa muigizaji wa mahiri "Bongo Movies" Steven Charles Kanumba (The Great). Tayari kuna filamu ambayo aliicheza siku chache kabla ya kifo chake ambayo inakwenda kwa jina la "NDOA YANGU" sasa imeingia madukani ikiwa inasambazwa na steps. Kulingana na uhalisia hii ndio filamu ya mwisho kuchezwa na Kanumba kwa kuwa sasa hatunaye tena duniani.


MUNGU AILAZE PEMA ROHO YA MAREHEMU

Tuesday, September 25, 2012

OLIC NA MANDZUKIC WALIJITABIRIA KUWA WATABADILISHANA TIMU???



Mara ya mwisho walipokutaka katika uwanja wa Allianz Arena msimu uliopita wa ligi ya Ujerumani (Bundesliga). Wachezaji Mario Mandzukic na Ivica Olic walikuwa wakichezea timu mbili tofauti na wanazocheza sasa. Ambapo Olic alikuwa Fc Bayern Munich na sasa amehamia Wolfsburg, na Mandzukic alikuwa VfL Wolfsburg na sasa amehamia Bayern. Jioni ya leo wawili hao wanatarajia kukutana tena kwenye uwanja wa Allianz Arena kwa mara nyingine wakiwa wamebadilishana timu. 

Wachunguzi wa mambo wanajiuliza je, walipobadilishana jezi katika msimu uliopita ni kama walikuwa wakitabiri kuwa watabadilishana timu baada ya msimu wa ligi kuisha? au kila mmoja alikuwa anaitamani timu ya mwenzie? kwa maana Olic alikuwa anatamani kuchezea Wolfsburg na Mndzukic alitamani kucheza Bayern???


Saturday, September 22, 2012

DIAMOND AIBIWA VIATU, KOFIA MPAKA SOKS DODOMA... LAKINI BADO AENDELEA NA SHOW BILA KUJALI

JAY MOE ATUA STOCKHOLM!!!! TAYARI KWA MAKAMUZI



Msanii wa Bongo Jay Moe a.k.a Mr, Mchopanga wakwanza kulia akiwa na masharobaro wa jiji la Stockholm pia wachezaji wa zamani wa the big team "Simba Sports" ya Dar. Kutoka kushoto ni Shekhan Rashid na Athuman Eid Machupa.

Habari za uhakika zinasema kuwa Jay Moe anatarajia kufanya makamuzi ya ajabu ndani ya jiji la Stockholm siku ya ijumaa ya tarehe 28 September 2012 kuanzia mida ya saa nne usiku mpaka majogoo.



KARIBU WEWE NA MWENZIO


DAVID ALABA APATA NAFUU




Lile jembe la ukweli kutoka kijiji cha vipaji maeneo ya Säbenerstr jijini Munich, makao makuu ya chama kubwa Fc Bayern. Kijana mwenye umri mdogo kuliko wote katika kikosi cha kwanza David Alaba ameanza kupata nafuu kutokana na majiraha aliyoyapata kwa zaidi ya mwezi sasa.

Alaba aliwadhihirishia mashabiki kuwa anaendelea vizuri pale alipoingia mazoezini asubuhi ya leo na kupasha misuli kwa kukimbia hapa na pale huku akiwasalimia mashabiki waliohudhuria mazoezini hapo.

Friday, September 21, 2012

NANI KUIBUKA MISS TEMEKE LEO???




Kusini mwa jiji la Dar es Salaam pembezoni mwa bahari ya hindi maeneo ya mtoni sabasaba kwenye ukumbi wa PTA. Jioni ya leo patamalizika ubishi wa kuwa ni nani atavalishwa taji na kuwa Miss Temeke 2012/13

Kama picha inavyojionyesha hapo juu, hao ni washiriki wa Miss Temeke ambao ni warembo waliorembeka hasa

ONLY 24 HRS REMAING TO GO.... OKTOBERFEST IN MUNICH




This is how the main gate  looks like by night



CHEERSS!!!!!!!!!!!!!!!




Wednesday, September 19, 2012

Tuesday, September 18, 2012

NGOMA AFRIKA BAND WAACHA GUMZO BREMEN


Ras Makunja na vijana wake wakiwasha moto

Ni kundi la muziki wa dansi linaloundwa na vijana wa ki Tanzania kwa kushirikiana na vijana wenzao kutoka Congo ambapo wote kwa pamoja wanaishi nchini ujerumani. Chini ya uongozi wa Captain Ras Makunja (mtanzania) juzi waliacha wakizungumziwa baada ya kutoa show ya nguvu katika mji wa Bremen nchini ujerumani. Kwa hakika walikonga nyoyo za mashabiki wariohudhuria na pia kuwakumbusha nyumbani wazungumzaji wa lugha ya kiswahili pale walipoimba nyimbo za kiswahili. Yani ilikuwa ni burudani ya aina yake.



Baadhi ya masahbiki waliohudhuria wakiserebuka na kujimwaga uwanjani kuburudika na burudani tamu ya Ngoma Afrika Band


Monday, September 17, 2012

PREZZO ABONGA NA SALAMA WA MKASI BAADA YA BIG BROTHER

J.B AMPIGIA SALUTI MPOKI WA ORIJINO KOMEDI




Ilikuwa ni kwenye Tamasha la Fiesta mjini morogoro, ndipo muigizaji maarufu Jcob Steven (mwenye fulana nyeupe wa kati) aliposhindwa kujizuia na kujikuta akienda kumwagia minoti baada ya kumvunja mbavu kwa vichekesho vyake. Mchekeshaji anaejulikana kwa jina la Mpoki kutoka kundi la Orijino Komedi au ukipenda unaweza kumwita mwarabu wa Dubay, maarufu kama mwarabu wa Libya au mwarabu mweusi, kwa kuokoa muda mwite bepari wa kihaya.

Sunday, September 16, 2012

DJ DULLY BOY KUWASHA MOTO NDANI YA MEMMINGEN NEXT SATURDAY



Jumamosi ijayo ya tarehe 22 Sptember 2012, mji wa Memminge katika jimbo la Bayern utakuwa na burudani ya muziki usiopimika kutoka kwa Dj Dully boy na Dj Rama. Bila kusahau the Most wanted "Dj Max" pia atawakilisha.

Burudani hii ni kuanzia mida ya saa tatu usiku mpaka asubuhi, pia kutakuwa na chakula cha ki Africa na vinywaji mbalimbali. Zawadi maalum zitatolewa na Mambo Bado sounds na Dj Max Entertainments kwa mwanadada atakaependeza kuliko wote, pia kwa watu watatu watakao cheza vizuri zaidi.

KARIBUNI SANA!!!!

ONLY 6 DAYS REMAINING... JAVI MARTINEZ IS READY FOR OKTOBERFEST




Ikiwa zimebaki siku 6 tu kuelekea kwenye Festival kubwa kuliko zote katika jimbo la Bayern (Oktoberfest), tayari kiungo mpya wa Fc Bayern "Javi Martinez" ameshanunua mavazi ya asili ya kibavaria kwa ajili ya tamasha hilo.

Tamasha hili hufanyika kipindi kama hiki kila mwaka kwa takriban muda wa wiki mbili na nusu, na kwa mwaka huu litaanza rasmi siku ya jumamosi ijayo 22 Sep 2012 mpaka tare 7 Okt 2012. Tamasha hili la wanywa Pombe linalojulikana kama Oktoberfest litafanyika maneneo ya Theresienwiese katika jiji la Munich.

MASHABIKI JINSI WALIVYOMCHOKOZA DIAMOND KWA KUTAJA JINA LA WEMA ALIPOIMBA KWENYE FIESTA DODOMA

Saturday, September 15, 2012

HAPPY BIRTHDAY TO YOU " DJ LADY KIARIE"




The Dj Max Entertainments and the crew wish you a happy birthday, we are very happy to work with you. May God bless you on this special day and forever. with lots of Love from my self (Dj Max). Me and my crew together we say 
HAPPY BIRTHDAY

Monday, September 10, 2012

BAADA YA BILBAO KUTAKA KUMUWEKEA NGUMU MARTINEZ HATIMAYE AANZA MAZOEZI RASMI NA FC BAYERN



Kifaa kipya cha Fc Bayern kikiwa kinatokea Bilbao, ambapo usajili wake almanusura ulete utata na labda asingeweza kuchezea nyota nyekundu ya kusini (FC BAYERN) hatimaye kila kitu kipo sawa na leo ameanza mazoezi rasmi. 

Picha juu inaonyesha akiwa na Bastian Schweinsteiger (kushoto) baada ya mazoezi wakibadilishana mawazo

Sunday, September 9, 2012

JUMA NATURE BADO NI NOMA!!!! AFUNIKA FIESTA TABORA KINOMA NOMA



Anaitwa Juma Kassim Kiroboto, mtoto wa Temeke jijini Dar. Ingawa wengi hupenda kumuita Juma nature au Sir nature. Pamoja na kuwa hajadondosha songi jipya kwa muda mrefu kidogo lakini pindi anapopanda jukwaani huwatia uchizi mashabiki wake wa masongi yake ya kitambo. Bado kuna watu wanajiuliza je? anatumia kizizi?

"Huyu jamaa hajatoa wimbo mpya lakini alipopanda tu watu wote walichanganyikiwa kwa furaha, sijui ana kizizi" moja ya mashabiki alisikika akisema baada ya tamasha la Fiesta lililofanyika mjini Tabora ambalo liliandaliwa na wakali wa burudani nchini Tanzania Clouds radio (the people station)

Saturday, September 8, 2012

JULIA NJOROGE FROM KENYA IS MISS EAST AFRIKA BELGIU 2012



Kwa niaba ya The Dj Max Entertainments and the crew, tunakupa hongera sana dada yetu kwa kushinda taji la Miss East Africa Belgium. Hongera pia kwa waandaji bila za kumsahau Azam, Kitokololo na the big bosss Denis Ruba

Wednesday, September 5, 2012

EAST vs WEST AFRICA PARTY IN MUNICH ILIKUWA NOMAA!!!!!


Super Dj Rama akifanya makamuzi



Bobby St akiwarusha mashabiki


Wadada warembooo!!!!!!!!!



Dj Lady Kiarie..... One Love!!!!



Cute girls


Just chilling and Enjoying



Mashabiki wakiburudika na kuburudishwa na Bobby st



Doctor Kingo in the house!!!!!!!  kaka rudi kazini wagonjwa watakufa



Hapa nimejichanganya na wenye Munich yao




NYOMI ZAIDI YA LILE!!!!!