Wednesday, January 23, 2013

HUSSEIN MACHOZI: "NILITAMANI KUWA MCHEZAJI MAARUFU LAKINI MAISHA YAMENIFANYA NIWE MWANAMUZIKI MAARUFU"



Mwanamuziki maarufu wa "Bongo fleva" leo hii amefunguka alipokuwa akifanya mahojiano na kipindi cha Leo tena cha Clouds fm. Akielezea historia ya maisha yake na shida alizokutana nazo mpaka kufikia hapo alipo leo hii, hadi kufanya jina lake halisi la Hussein Rashid kubadilika na kuwa "HUSSEIN MACHOZI"

Akielezea ndoto zake za kucheza timu ya taifa ya mpira wa miguu ya Tanzania pia alifunguka kwa kusema kuwa kocha msaidizi wa sasa wa timu ya taifa (Jina kapuni) ndiye aliyevunja ndoto zake za kuendeleza kipaji chake cha mpira wa miguu wakati akiwa timu ya Kagera Sugar. Miongoni mwa vitu alivyokuwa akifanyiwa na kocha huyo na kumkatisha tamaa ni kupewa nguo za kocha huyo ali amfulie wakati wachezaji wengine wakiendelea na mazoezi.

Hata hivyo aliendelea kusema kuwa bado anaupenda sana mchezo wa mpira wa miguu kuliko muziki lakini hali ya maisha kwa sasa hamruhusu, labda kama atapata timu ambayo itamlipa vizuri.

No comments:

Post a Comment