Tuesday, January 15, 2013

MSANII LADY JAY DEE AMALIZA SALAMA SAFARI YA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO


Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka nchini Tanzania na pia mmiliki wa kundi la muziki la Machozi Band, Judith Wambura "LADY JAY DEE" ukipenda unaweza ukamwita Jide. Amemaliza salama safari yake ya siku sita ya kukwea kilele cha mlima mrefu kuliko yote barani Afrika "Mlima Kilimanjaro" akiwa ameongozana na mumewe pamoja na mpiga picha wao. Mara baada ya kushuka kutoka kileleni walikabidhiwa vyeti maalum vya uthibisho kuwa wamefika kilelena. Vyeti hivyo walikabidhiwa na muhifadhi mkuu wa mlima huo.

No comments:

Post a Comment