Tuesday, September 4, 2012

BI KIDUDE HAJAFAAAA!!!!! WACHENI KUMZUSHIA




Msanii maarufu na mzee kuliko wote Afrika mashariki, ambae ni mzaliwa wa Zanzibar katika Jamhuri ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar (TANZANIA). Fatma bint Baraka maarufu kama bi Kidude alizushiwa kuwa amefariki mwishoni mwa juma lililopita baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Taarifa za sahihi kutoka kwa wajukuu zake zinasema kuwa bibi bado yuhai  na kwa uwezo wa mungu ataishi maisha marefu zaidi japokuwa kwa sasa afya yake si nzuri kutokana na kusumbuliwa na maradhi ambayo hawakuyataja. "Maradhi ni kitu cha kawaida na kila binaadamu huugua, ni kweli bibi anaumwa lakini hajafa na tunamuombea kwa mungu apate afueni" hayo yalisemwa na mjukuu wake ambaye pia ni msanii wa miondoko ya mduara kutoka visiwani nilipoongea nae kwa njia ya simu, lakini aliomba jina lake lisiandikwe hapa, nami nafanya hivyo kwa kumuheshimu na kuheshimu mawazo yake.




No comments:

Post a Comment