Sunday, September 30, 2012

MUANZILISHI WA BONGO FLEVA APATA MTOTO



Miongoni mwa wasanii wa awali kabisa kutambulika katika ramani ya muziki wa kizazi kipya mwanzoni mwa miaka ya tisini, Joseph Mbilinyi "Mr too proud au Sugu" ambaye kwa sasa ni mbunge wa jimbo la Mbeya mjini kupitia chama cha Chadema. Sasa amekuwa baba baada ya mwenyezimungu kumjaalia neema ya mtoto.

Pia ifahamike kuwa Sugu ndio msanii mwenye Album nyingi zaidi kuliko kuliko msanii mwingine yoyote wa bongo fleva. Vilevile ni msanii wa kwanza kutoa album na ndiye aliyekuwa msanii wa kwanza wa bongo fleva kupata nafasi ya kupiga "show" barani ulaya



Huyu ndiye mtoto wa Sugu, kwa jina anaitwa Sasha. Mungu ambariki na kumkuza vizuri


No comments:

Post a Comment